Ligi Kuu ya soka ya NBC Tanzania bara inaendelea tena leo Agosti 29 kwa mchezo mmoja ambapo Mabingwa watetezi wa Ligi hiyo Yanga SC wachachuana na Mabingwa wa Championship 2022/23 JKT Tanzania katika dimba la Azam Complex Chamazi.
Yanga SC vs JKT Tanzania
Azam Complex, Chamazi
saa 1:00 jioni
Yanga na JKT Tanzania ni miongoni mwa timu chache ambazo hazijaruhusu goli kwenye NBCPL msimu huu wa 2023/24 sambamba na, Singida Fountain Gate FC, Mashujaa FC na Geita Gold FC.