Home Habari za michezo YANGA WAFUNGUKA UWEPO WA GAEL BIGIRIMANA KAMBINI

YANGA WAFUNGUKA UWEPO WA GAEL BIGIRIMANA KAMBINI

Afisa Habari wa Yanga SC Ally Kamwe

Uongozi wa Yanga umeelezea sababu ya aliyekuwa nyota wao Gael Bigirimana kuonekana kambini Avic Town ni kusalimiana na wenzake.

Akizungumzia ishu hiyo leo Agosti Mosi, 2023, Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe, alisema Gael ni familia ya Yanga hivyo alifika kambini kuwasalimia wachezaji wenzake.

“Alikuja kuwasalimia ndugu zake, sisi Yanga ni familia. Anafanya mazoezi na wenzake lakini sio mchezaji wa Yanga, ni kama vile Aziz Ki alivyokwenda kupasha na ASEC Mimosas,” alisema Kamwe.

SOMA NA HII  HIKI HAPA KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA RUVU SHOOTING