Home Uncategorized TANZANIA PRISONS KUMCHOMOA MSHAMBULIAJI MMOJA WA SIMBA

TANZANIA PRISONS KUMCHOMOA MSHAMBULIAJI MMOJA WA SIMBA

NYOTA wa Simba, Marcel Kaheza kwa sasa yupo kwenye hatua za mwisho kujiunga kwenye kikosi cha Tanzania Prisons.

Kaheza amemalizana na AFC Leopards ya Kenya alikokuwa anakipiga kwa mkopo kwa sasa yupo Dar habari zimeeleza kuwa anawinwa na Prisnons.

Mmoja wa kiongozi wa Tanzania Prisons amesema kuwa walianza kufanya mazungumzo na Kaheza kabla ya kutua Simba akitokea MajiMaji FC.

“Tulianza kufanya mazungumzo na Kaheza muda mrefu kabla ya kutua Simba akitokea Majimaji hivyo kwa sasa bado yupo kwenye mipango ya timu,” alieleza.

Kaheza amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kurejea Kenya hesabu zake ni kupata timu hapa Bongo ili kuendeleza kipaji chake.

SOMA NA HII  ONYANGO: KAHATA KANILETA SIMBA SC