Ratiba ya michuano hiyo imepangwa Septemba 2, 2023 ambapo Simba inatarajiwa kuanza kwa kuikaribisha Al Ahly ya Misri, mchezo wa kwanza ukitarajiwa kuchezwa Oktoba 20, 2023 kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam
Michuano hiyo inayosimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) pia inatambulika kwa jina la African Football League, inashirikisha timu 8, inaanzia hatua ya Robo Fainali ikiwa katika mfumo wa mtoano
Mechi nyingine za Robo Fainali; TP Mazembe vs Espérance Sportive de Tunis, Enyimba FC vs Wydad Athletic Club, Atlético Petróleos de Luanda vs Mamelodi Sundowns