Habari za michezo
YANGA -TUNATAKA CHANGAMOTO YEYOTE….. ANAETUWEZA AJE…
Staff Desk
September 5, 2023
2:37 pm
Klabu ya Yanga imesema kuwa wakati huu ambapo ligi imesimama wanataraji kucheza mchezo wa kirafiki siku ya Jumapili lakini jina la timu bado halijawekwa hadharani.
Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe amesema pia wanatoa nafasi kwa timu yoyote ambaoyo wanajiona kuwa wana uwezo wa kushindana na Yanga basi wacheze mahala popote pale.
Akizungumza Ally Kamwe amesema;
“Tunatarajia kuwa na mchezo wa kirafiki siku ya jumapili. Tutatangaza tunacheza na timu gani. Hata hivyo tunatoa fursa kwa timu yoyote inaweza kuomba mchezo wa kirafiki na sisi tutacheza popote pale”
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.