Baada ya Simba kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Power Dynamos jana Septemba 16 nchini Zambia katika Dimba la Levy Mwanawasa.
Meneja wa habari na mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally kupitia ukurasa wake wa instagram ameandika;
“Sare yenye manufaaa kwetu, ingawa tungeweza kupata ushindi mkubwa zaidi kama tungetumia kila nafasi tuliyoipata lakini huo ndo mpira Asante Power Dynamos kwa kutupa mchezo mzuri wenye hadhi ya Ligi ya Mabingwa Afrika Karibuni Dar es Salaam tuje tumalizane Leo ilikua ni siku ya kusoma Mashtaka, October 1 ni siku ya hukumu”.