Habari za Michezo
Azam FC

FEI TOTO, DUBE WATAKIWA KUJITOA AZAM, DABO ASEMA HAYA

Staff Desk September 17, 2023 2:17 pm

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Yousouph Dabo, amesema kikubwa ambacho wachezaji wake wanatakiwa kukifanya ikiwa ni pamoja na kiungo Feisal Salum na mshambuliaji Prince Dube ni kujitoa muda wote kutafuta ushindi.

Dabo ambaye ameiongoza Azam kucheza mechi mbili za Ligi Kuu Bara msimu huu na kushinda zote, amesema: “Kwa namna ambavyo tunafanya maadalizi kwa mechi zijazo ni muhimu kwa wachezaji kucheza kwa kujitoa zaidi ili kupata matokeo mazuri uwanjani.

“Tunaamini kuna makosa ambayo yanatokea, hayo tunayafanyia kazi ili kuwa imara kwa mechi zijazo. Ushindani ni mkubwa, hilo lipo wazo nasi tunajitahidi kufanya kazi nzuri kupata matokeo,” alisema Dabo.

Mchezo ujao kwenye Ligi Kuu Bara, Azam FC inatarajiwa kucheza Septemba 21, mwaka huu dhidi ya Singida Fountain Gate.

HUKO LIGI KUU MAMBO NI MOTO, SIO SIMBA, YANGA WALA AZAM, MWAMBA HUYU HAPA CHAMA AGEUKA DHAHABU KWENYE MCHEZO WA SIMBA ZAMBIA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply