Habari za michezo

BAADA YA KUANZA VIBAYA NYONI AFUNGUKA MIPANGO YA NAMUNGO

Staff Desk September 26, 2023 7:01 pm

Kiungo wa Namungo FC, Erasto Nyoni amesema licha ya kuanza vibaya michezo yao ya Ligi Kuu Tanzania Bara lakini anaamini watafanya vizuri msimu huu 2023/24.

Kiungo huyo amesema kinachompa imani hiyo ni aina ya wachezaji waliosajiliwa na timu hiyo na uzoefu waliokuwa nao.

Timu yetu ina wachezaji wengi wenye uzoefu na ligi, lakini pia hata benchi letu la ufundi lipo vizuri ndio maana matumaini ya Namungo kufanya vizuri msimu huu kwangu ni makubwa,” amesema Nyoni.

Mkongwe huyo aliyewahi kutamba na miamba ya soka nchini Simba SC, amesema baada ya kupata pointi moja kwenye mechi tatu walizocheza za ligi mpango wao ni kuhakikisha wanashinda mechi zinazofuata.

Nyoni amesema yeye na wachezaji wenzake wamejipanga kuhakikisha wanabadilisha matokeo mabaya na kupata ushindi ambao utatimiza malengo ambayo wamedhamiria kuyafikia msimu huu.

Malengo ya Namungo FC msimu huu ni kumaliza ligi kwenye nafasi tatu za juu ili kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao 2024/25.

ELCLASICO ILIANZA LINI!? NANI ANAONGOZA KWA REKODI!? AL MAREIKH HAWA HAPA NCHINI KWAAJILI YA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply