Home Habari za michezo MASTAA HAWA WA YANGA WANAFAA PALE SIMBA KABISA

MASTAA HAWA WA YANGA WANAFAA PALE SIMBA KABISA

Unajua kwa nini Simba SC walipewa jina na Lunyasi na Yanga walipewa jina la Kudere.

Iko hivi Simba walipewa Lunyasi kwa sababu walikuwa wanaweka mpira chini (lilikuwa linapigwa Samba).

Yanga wao waliitwa Wazee wa Kudere kwa sababu walikuwa ni daima mbele nyuma mwiko, yaani wao wanawaza kwenda mbele ndio maana walikuwa wanapiga tu mipira mbele na walikuwa na mawinga vibendera.

Kwa sasa kuna baadhi ya wachezaji ndani ya kikosi cha Yanga nikiwatazama naona kabisa wana-fit katika soka la Simba ambalo lina utamaduni wa pasi nyingi alafu fupi fupi hadi wanafika goli la mpinzani.

Max Nzengeli, Zouzoua Pacome, Aziz Ki na Khalid Aucho hawa ni wachezaji ambao wangekuwa wanacheza vizuri zaidi ya sasa walivyokuwa kama wangekuwa wapo katika kikosi cha pili.

SOMA NA HII  MAFURIKO YA RWANDA YANGA WAFANYA HAYA