hafiz konkani
Habari za michezo

HUYU HAPA MRITHI WA KONKANI YANGA

Staff Desk October 9, 2023 3:58 pm

Taarifa kutoka ndani ya Klabu Yanga zinaeleza kuwa, timu hiyo inahusishwa kumnyemelea mshambuliaji wa Gor Mahia, Benson Omalla Ochieng katika usajili wa dirisha dogo mwezi Januari ili kuimarisha safu yao ya ushambuliaji.

Omalla ambaye ni raia wa Kenya amekuwa na kiwango kizuri tangia msimu uliopita na msimu huu, alikuwa chaguo la pili la Yanga baada ya Hafiz Konkoni wakati wa usajili lakini hatimae Yanga wakamsajili Hafiz Konkoni kutoka Becham ya Ghana.

Hata hivyo, Mghana huyo ameshindwa kuonesha makali yake na huenda akatolewa kwa mkopo katika dirisha dogo la mwezi Januari.

Yanga pia wanaye mshambuliaji kutoka Zambia, Kennedy Musonda aliyesajiliwa katika dirisha dogo la msimu uliopita lakini bado hajaonyesha makali kama ambavyo Yanga walitarajia na badala yake washambuliaji wote hao wamekuwa wakiwekwa benchi na mzawa, Clement Mzize.

SIMBA, YANGA MSIBWETEKE KIMATAIFA ROBERTINHO ATAMBA AWAPA NENO HILI MASHABIKI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6131

Leave a Reply