Habari za Simba
Habari za michezo

AL AHLY ATAKUBALI KUENDELEZA UTEJA DHIDI YA SIMBA LEO AFL

Staff Desk October 20, 2023 8:19 am

Leo dunia ya soka itahamia Tanzania katika Uwanja wa Benjamin Mkapa. Ni katika uzinduzi wa michuano mipya ya African Football League ambapo pamoja na shamrashamra za ufunguzi wake, kutapigwa mechi ya kiume kati ya Simba na Al Ahly kutoka Misri.

Simba imekuwa timu tishio kwa siku za hivi karibuni, ikiwa imefanya makubwa kwenye soka la Afrika, iliitangaza kuwa timu ya saba kwa ubora baada ya kufika robo fainali mara tatu mfululizo ya Ligi ya Mabingwa na mara moja Kombe la Shrikisho.

Simba wamekuwa bora wanapocheza na Ahly Kwa Mkapa, wakiwa wamekutana nao mara nne na kupata ushindi wa asilimia 100, yaani walishinda michezo yote na huu utakuwa mchezo wa tano wanakutana.

UNYAMA MWINGI….REKODI ZAIBEBA SIMBA UKIACHANA NA KIPUTE CHA SIMBE LEO….YANGA WAINGIA MTEGO WA AZAM FC….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply