Taifa Stars
Habari za michezo

KUELEKEA MECHI NA NIGER…TAIFA STARS MAMBO NI ‘NGINJA NGINJA’….

admin November 17, 2023 6:57 pm

KOCHA Mkuu wa Timu ya Taifa Tanzania, Taifa Stars Adel Amrouche ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Niger.

Stars itakuwa na kibarua cha kusaka ushindi huo na imewasili salama Morocco kwa ajili ya mchezo huo kwa ndege iliyotolewa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu.

Maandalizi yameanza ambapo mazoezi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Grand Marrakech Annex 1, Morroco kuelekea mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Niger utakaochezwa kwenye mji wa Marrakech Jumamosi Novemba 18, 2023.

Kocha huyo amesema: “Tunafurahi kuwa hapa na kufika salama na maandalizi ya mchezo wetu ambao utakuwa na ushindani mkubwa.

“Mchezo mgumu na mpira unahitaji matokeo ya furaha hicho ndicho ambacho ninakijua hivyo nina amini itakuwa hivyo mashabiki watafurahi,”.

MERIDIANBET WAGAWA REFLECTORS KWA DEREVA BODABODA NA BAJAJI.. MASTAA SIMBA, YANGA WAIJAZIA MAMILIONI TFF…’ISHU’ NZIMA IKO HIVI…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply