Habari za Yanga
Habari za michezo

YANGA WASHINDWA KUTAMBA UGENINI, WAPOKEA KIPIGO KIZITO

Staff Desk November 25, 2023 6:31 am

MABINGWA wa Tanzania, Yanga SC wameanza vibaya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuchapwa mabao 3-0 na wenyeji, CR Belouizdad usiku huu Uwanja wa Julai 5, 1962 Jijini Algiers nchini Algeria.

Mabao ya CR Belouizdad katika mchezo huo wa Kundi D yamefungwa na kiungo Abdelraouf Benguit dakika ya 10 na washambuliaji, Abderrahmane Meziane Bentahar dakika ya 45 na ushei na Mgambia Lamin Jallow dakika ya 90 na ushei.

Mechi nyingine ya Kundi D itachezwa kesho baina ya wenyeji, Al Ahly dhidi ya Medeama Ghana Uwanja wa Al Ahly Jijini Cairo nchini Misri.

Yanga watashuka tena dimbani Desemba 2 kumenyana na mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam na CR Belouizdad watasafiri hadi Ghana kucheza na Medeama.

MTOKO WA WENYENCHI,KOCHA WA MAKOMBE APEWA TIMU AFUNGUKA KWELI NJIA NI NGUMU ILA INAPITIKA MBONA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply