Habari za michezo

HUU MPANGO WA SIMBA WAWATISHA MABEKI WYDAD

Staff Desk December 8, 2023 2:27 pm

Wakati klabu ya Simba ikiendelea na maandalizi kabla ya kuivaa Wydad Casablanca kesho jijini Marrakech, Morocco huku beki wa timu ya Wydad, Arsene Zolla akionekana kuingiwa ubaridi kwa kuihofia Simba.

“Unakumbuka tulivyocheza nao huku mara ya mwisho walionyesha mchezo mkubwa lazima unapokwenda kukutana na timu kama hiyo mnatakiwa kuwa makini,” alisema Zolla.

“Wana wachezaji waliokomaa sana na mashindano kama haya na unaona sasa wamemuongeza ndugu yangu Fabrice (Ngoma) ni mchezaji mkubwa tunamjua na anaijua Wydad utaona kwamba timu yao sio mbaya.” Aidha Zolla aliongeza hatua ya kikosi cha Wydad kushinda mabao 3-1 mechi ya Ligi Kuu mbele ya Mouloudia Oujda, ni hatua nzuri ya kujiandaa na mchezo huo wa kesho wakiwa na morali.“Tulikuwa hatujashinda mechi nne mfululizo, lakini sasa angalau tumepata nguvu kuikabili Simba.”

TANZANIA U18 YATAMBA UBINGWA CECAFA SIMBA YAIFANYIA UMAFIA WYDAD… BECHI LA UFUNDI LAKIRI JAMBO HILI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply