Home Habari za michezo WAKATI YANGA WAKIMALIZANA NA OKRAH JUZI….WATURUKI KUMNYOFOA DIARA JANGWANI…

WAKATI YANGA WAKIMALIZANA NA OKRAH JUZI….WATURUKI KUMNYOFOA DIARA JANGWANI…

Tetesi za Usajili Yanga leo

Tetesi kutoka kwenye chanzo Cha kuaminika kutoka nchini Mali kuhusu Kipa wa Yanga SC Djidui Diarra zinasema Kuna timu ya ligi nchini Uturuki inahitaji huduma ya golikipa Huyo Bora ndani ya Africa akiwa amefanikiwa kutwaa tuzo ya golikipa Bora mara mbili ya ligi kuu,lakini akitwaa tuzo ya kipa Bora kwenye fainali kombe la shirikisho fainali dhidi ya USM Alger.

Wamevutiwa na ubora wa kipa Huyo baada ya kuingia kwenye kinyang’anyiro Cha kugombea kipa Bora katika tuzo za CAF na makipa wakubwa Afrika lakini pia amekuwa akitwa kwa muendelezo katika timu ya taifa ya Mali.

Lakini ukiacha yeye timu hiyo pia imevutiwa na mchezaji mwingine kiungo kutoka Mali Aliou Dieng kutoka klabu ya Al Ahly ya Misri nae akitakiwa kwenda kwenye hiyo klabu ya Uturuki pamoja na Screen protecter Diarra.

Itakumbukwa kuwa, Diara aliyekuja nchini miaka mitatu iliyopita ameendelea kuwa nguzo imara kwa klabu yake na timu yake ya Taifa , ambapo moja ya mafanikio makubwa aliyoyapata hivi karibuni ni kuvaa medali ya shaba kwenye kombe la shirikisho mwaka jana.

SOMA NA HII  PAMOJA NA KUONYESHA KIWANGO KIKUBWA...SAIDO MBIONI KUIKIMBIA YANGA...ISHU YA MKATABA YATAJWA...