Home Habari za michezo TAIFA STARS KUSHIRIKI MASHINDANO MAPYA YA FIFA….MCHONGO KAMILI UKO HIVI…

TAIFA STARS KUSHIRIKI MASHINDANO MAPYA YA FIFA….MCHONGO KAMILI UKO HIVI…

Habari za Michezo leo

Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” inatarajia kwenda nchini Azerbaijan Kwaajili ya mashindano madogo ya FIFA Series yatakayo husisha timu nne kutoka mabara tofauti.

Stars itacheza mchezo wake wa kwanza March 22 dhidi ya Bulgaria na mchezo wa pili utapigwa March 25 dhidi ya Mongolia.

FIFA Series ni mashindano madogo mbadala wa mechi za kirafiki za kimataifa timu shiriki zitakuwa ni Tanzania, Bulgaria, Mongolia pamoja na mwenyeji Azerbaijan.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Tanzania kushirikishwa kwenye mashindano hayo yanayoandaliwa na FIFA kwa mara ya kwanza pia katika kutimiza kalenda ya michezo ya kimataifa.

Mbali na Azerbaijan, FIFA pia wameandaa michezo hii kwenye mataifa ya Saudi Arabia, Algeria, Sir Lanka,

Baadhi ya nchi za kiafrika zitakazoshiriki ni pamoja na Tanzania, Zambia, Ghana , Afrika Kusini , Algeria na Ethiopia.

Bado haijawekwa wazi kama mashindano haya yatakuwa na zawadi au kitu chochote cha kuwapongeza washindi wa jumla.

SOMA NA HII  IHEFU KUITIBULIA TENA YANGA...MIPANGO YAO LAZIMA KINA SKUDU 'WAOMBE POO'...