Home Habari za Yanga WABABE WA YANGA WAANZA TAMBO…KUMBE WALIMFANYIA MAZOEZI SPESHO AZIZ KI

WABABE WA YANGA WAANZA TAMBO…KUMBE WALIMFANYIA MAZOEZI SPESHO AZIZ KI

HII SASA NOMA... YANGA YAMPANDISHA SANGOMA NDEGE...JEMEDARI SAID AFUNGUKA A-Z

Kocha Msaidizi JKT Tanzania George Mketo amesema walifanya mazoezi ya kuwakaba Yanga wachezaji wao hatari akiwemo Aziz ki akiwa anatokea pembeni ndio maana waliwapanga walinzi watatu ili kuwazuia Yanga SC na waliingia kwenye mchezo kupata matokeo ya alama tatu lakini wamepata sare ni alama kubwa kwao kama Jkt Tanzania.

Mketo amesema hayo wakati akizungumza na wanahabari baada ya mchezo wao dhidi ya JKT kumalizika na kutoa sare ya bila
kufungana katika Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni, Dar es Salaam.

“Tuliwasoma Yanga michezo mitatu nyuma tukajua wapi yalipo madhaifu yao, walitegemea mashambulizi yao mengi kupitisha pembeni na mianya hiyo tuliziba.

Mtu mwingine hatari ni Aziz Ki ambaye akitoka pembeni akaingia ndani anatengeneza shuti au pasi ya hatari, ndiyo maana tukaweka mabeki watatu wa kati kuziba huo mwanya.

“Wachezaji wangu wameufuata mpango tuliowaelekeza na kuufanyia mazoezi kwa wiki mbili. Tulihitaji alama tatu lakini tulikuwa na malengo ya alama moja, tulisema tukikosa alama tatu basi tupate moja ambayo imewezekana kuipata katika uwanja wetu wa nyumbani.

“Tuliamini Yanga watakuja na viungo watatu, washambuliaji watatu na ndicho walichokuja nacho. Niliwapa kazi maalum Kapalata, Machezo na hamisi Ndemla na kuwazuia wasipige mashuti nyuma ya

SOMA NA HII  BENCHI LA UFUNDI YANGA LAMBANIA PACOME...ALI KAMWE AMEFUNGUKA HAYA A-Z