Habari za michezo

JUMA MGUNDA…AKABIRIWA NA MTIHANI HUU MZITO SIMBA…ISHU NZIMA IKO HIVI A-Z

Marce Ben Komba May 2, 2024 10:20 am

Wekundu wa Msimbazi Simba SC kesho watakuwa na kibarua kingine cha kujiuliza baada ya kupata sare katika mchezo uliopita.

Simba ambao kwa sasa inaongozwa na Kocha Juma Mgunda baada ya aliyekuwa kocha wake Abdelhak Benchikha kuomba kuondoka, itakuwa mwenyeji wa mchezo huo wa raundi ya 16.

Endapo Simba ataibuka ma ushindi atafikisha alama 50 na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kupambania nafasi ya pili dhidi ya Azam FC ambaye ana alama 54 akiwa mbele kwa mchezo mmoja.

Kwa upande wa Mtibwa akishinda, atajiweka kwenye nafasi nzuri ya kujinusuru kushuka daraja kwani kwa sasa yupo nafasi ya mwisho kwenye msimamo akiwa alama 17.

AHMED ALLY AWACHONGEA YANGA TFF…USHINDI WAO UCHUNGUZWE…ATEMA CHECHE HIZI KIBU DENIS AGOMA KUSAINI MKATABA MPYA SIMBA…DUH!! KUMBE ANA OFA HII MPYA  BONGO