Habari za Simba Leo
SIMBA YAKUTANA NA AUBIN KRAMO…ONANA AKALIA KUTI KAVU.
Abubakar
July 12, 2024
11:56 am
HABARI zilizotufikia hivi punde kuhusu hatma ya Winga hatarii Aubin Kramo na kinachoendelea kuhusu kuendelea kusalia kubaki Simba kwa msimu ujao.
Inaelezwa kwamba Aubin Kramo bado yupo Tanzania na alikuwa nana kikao cha kwanza na viongozi wa Simba siku ya Jumanne Julai 9.
Msimamo wa klabu ya Simba inataka Aubin Kramo apunguze mshahara wake kisha wamtoe kwa mkopo lakini inaonekana kuwa haiwezekani kwa upande wa mchezaji na wakala wake.
Madai ya mchezaji mwenye Kramo anataka nafasi ya kujidhihirisha Simba kwani anaamini kwa sasa yupo fiti kuchea na anaweza kuipambania Simba kufikia malengo yake.
Kikao cha pili kitafanyika kesho Julai 13 kabla Kramo hajarejea nyumbani kwao Ivory Coast siku ya Jumatatu kuendelea na maisha yake mngine. Ikiwa baada ya mkutano wa kesho na bado Simba hawajabadilisha mawazo yao, Kramo ataondoka klabuni.
Wakari yote haya yanatokea klabu ya Al Ahli wameonyesha nia lakini bado wanacheza mechi za mchujo za ligi ya Libya, hivyo waasubiri hadi watakapomaliza na kama Simba wakiachana na Kramo basi wao wapo mstari wa mbele kumpata mchezaji huyo.
Klabu ya US Monastir pia wamejiunga na wale wanaotaka kumsaini Kramo.
Kuhusu winga matata wa Cameroon Willy Esomba Onana juu ya hatma yake Simba iko hivi.
Bado yupo nyumbani na hajaitwa tena na klabu, wakati huo Wakala wake anatafuta fursa tofauti kwa ajili yake. Amepandwa kwa klabu kadhaa.
Elie Mpanzu Je ::
Kwa upande wa mchezaji mwenyewe inaonekana anataka Simba, hakuna kilichobadilika katika fikra zake licha ya Rais wa AS Vita Amadou Diaby kumshawishi abakie klabuni hapo.
Klabu hizo mbili ziko kwenye mawasiliano ya moja kwa moja na wanajaribu kukubaliana jambo lakini si rahisi. AS Vita wanafanya mazungumzo kuwa magumu sana.