Home Habari za Yanga Leo YUSUF MANJI ATAKUMBUKWA KWA MENGI YANGA…KUNA HAYA BAADHI.

YUSUF MANJI ATAKUMBUKWA KWA MENGI YANGA…KUNA HAYA BAADHI.

Yusuf Manji Yanga

YANGA INALIA Imempoteza Tajiri na mtu wa muhimu kwao, Tanzania inasikitika kumpoteza moja ya mtu muhimu, Simba inahuzunika kwa msiba wa Yusuf Manji kama mdau wa michezo na mtu aliyeleta ushindani wa Simba na Yanga.

Wakati ambao masikio na macho hayataki kuamini kile inachokisikia na kukiona, huo utabki kuwa ukweli, Dunia imempoteza mtu wa mpira ni msiba wa wote kwa wapenzi wa mpira.

Lakini Yanga watakuwa wanalia kwa mengi sana, ukiachana tu na uwekezaji uliofanywa na Tajiri Yusuf Manji, alikuwa ni zaidi ya Mwanafamilia wa Yanga.

Manji alikuwa zaidi ya Mwekezaji, Zaidi ya Ndugu , Zaidi ya Mwanayanga Mbele ya Wanayanga Wenzake.

MAMBAO AMBAYO MANJI ATAKUMBUKWA NAYO AKIWA YANGA.

(1) Manji aliwai kuwalipia Viingilio Mashabiki wa Yanga Mechi ya Yanga na TP MAZEMBE, Mashabiki na Wanachama Wakaingia Bure.

(2) Manji Aliwalipia Viingilio Wanachama Wa Yanga kwa Ajili yakwenda Kuangalia Mechi ya Brazil na Taifa Stars, Brazil ya Akina Kaka.

(3) Manji alianzisha Week ya Wananchi na Kila Jumamosi kwa Miezi Miwili, Mashabiki na Wanachama wa Yanga Walikuwa Wakikutana Viwanja vya Mnazi Mmoja Wakila na kunywa gharama zote Zikibebwa na Yusufu Manji.

(4) Manji alishawahi kukodi Ma-Bus nakusafirisha Wanachama wa Yanga kutoka Dsm Kwenda Morogoro kuishangilia Yanga.

(5) Manji alishawahi kuwalipia Ada ya Uanachama Wanachama Wote wa Yanga kwa Mda wa Miaka Mitatu.

(6) Kipindi Hiko Jengo la Yanga likiwa Limechakaa zaidi, Manji aliweza kulifanyia Ukarabati nakulirudishiwa Muonekano Wakupendeza.

(7) Manji Aliwapa Yanga sehemu ya Ardhi ambayo Alikuwa anaimiliki Kigamboni ili Waweze Kujenga Uwanja Wao.

(8) Manji alikuwa na Vision kubwa sana na Yanga lakini Pia Yanga ilikuwa Moyoni mwa Manji.

(9) Manji ndiye Tajiri wa kwanza kupandisha Thamani ya Usajili na Mishahara kwa Wachezaji Nchini Tanzania.

Manji alisimama kama Kigezo na Kipimo Cha Mwekezaji yeyote Ndani ya Yanga na Simba

Kuna heshima yakipekee Yusufu Manji anastahili kwenye Soka letu.

Tajiri Manji alifariki akiwa anapatiwa matibabu nchini Marekani alipokuwa anaumwa kwa muda, Baada ya kuondoka Yanga Manji alibadilisha sehemu ya maisha yake yakawa New York Marekani.

SOMA NA HII  SURE AFUNGUKA MAZITO YANGA.