Habari za Yanga Leo
IBRAHIM BACCA ATWAA TUZO YA BEKI BORA.
Abubakar
August 2, 2024
10:52 am
Beki wa kati wa Yanga SC na Timu ya taifa ya Tanzania, Ibrahim Bacca ameshinda tuzo ya beki Bora wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara msimu wa 2023/24.
Bacca amewashinda wachezaji kadhaa akiwemo beki wa kushoto wa Simba Mohammed Hussein Tshabalala, ambaye alikuwa kwenye kinyang’anyiro kimoja na mwamba huyo.
Ibrahimu Bacca tangu atue Yanga msimu wa tatu sasa akitoea Zanzibar, amekuwa na kiwango kizuri kdri siku zinavyozidi kwenda.
Licha ya makocha anga kubadilishwa kutoka enzi za Nasradinne Nabi hadi Miguel Gamondi, Bacca amekuwa na uhakika wa kuanza.