“Hakuna kinachoshindikana mpira ni mchezo wa makosa dakika 90 zenye mbinu bora na sahihi zitatupa matokeo mazuri ugenini tunaheshimu ubora wa wapinzani wetu na wao wasitarajie mteremko kutoka kwetu,” amesema Muya na kuongeza;
“Tunafahamu imetoka kupoteza taji la Mapinduzi kwa mikwaju ya penati hawatataka kurudia makosa kwa kupoteza pointi tatu Ligi kuu na sisi tumejiandaa kuonyesha ushindani dhidi yao hivyo utakuwa mchezo mzuri na wa ushindani.”
Kocha huyo alisisitiza; “Tutaingia kwa tahadhari na kuwaheshimu wapinzani wetu ni timu ambayo ina historia ngumu kwetu tangu imepanda tukikutana huwa mchezo unakuwa mgumu timu bora ndio inaamua matokeo.”
“Tunatarajia mechi ngumu na ya ushindani tumejiandaa vizuri na tunatarajia matokeo mazuri kwenye mchezo wa huo kutokana na mipango ya benchi la ufundi sambamba na wachezaji wenyewe,” aliongeza.
Rekodi inaonyesha katika mechi ya mwisho uwanjani hapo msimu uliopita timu hizo zilipokutana katika Ligi Kuu, wenyeji Azam ilishinda kwa bao 1-0 na ziliporudiana zilitoka suluhu, lakini katika mechi ya nusu fainali ya Ngao ya Jamii 2024, Azam iliifunga Coastal 5-2