Barabara Za AFCON Mbioni Kukamilika
BARABARA zinazoelekea katika Mji wa AFCON uliopo Fumba, zinatarajiwa kukamilika Desemba mwaka huu kwani mradi huo unategemewa kufungua fursa za kiuchumi kisiwani hapa.
“Ujenzi wa barabara hii utakamilika mwezi Desemba na itaanza kutumika rasmi kati ya Januari au Februari 2027,” amesema.
Makamu huyo, amesema kukamilika kwa barabara hizo kutarahisisha maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) itakuwa kichocheo kizuri cha ukuaji uchumi na uwekezaji Zanzibar.
Alieleza kuwa tangu kuanza kwa ujenzi huo, Fumba imeshuhudia mabadiliko makubwa ya uchumi ikiwemo kuongezeka kwa thamani ya ardhi na wananchi kunufaika na mradi huo.
Naye, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar, Dk Khalid Salum Mohamed amesema wizara hiyo inalenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwezi Februari 2027 miundombinu yote ianze kutoa huduma.