Uncategorized

YANGA WAPEWA BURE MBADALA WA MAKAMBO

admin May 31, 2019 11:34 am


UONGOZI wa Mwadui FC umesema kuwa upo tayari kuwapa nyota wao Salum Aiyee hata bure endapo watakuwa wanahitaji saini yake msimu ujao.

Yanga kwa sasa inatafuta mbadala wa Heritier Makambo ambaye amesepa Yanga akiwa amefunga jumla ya mabao 17 msimu huu na kujiunga na kikosi cha Horoya ya Guinea huku Aiyee akiwa na mabao 18.

Katibu wa Mwadui FC, Ramadhan Kilao amesema kuwa kwa sasa ahawajona dalili za Yanga kumfuata nyota huyo kama ikitokea wataketi kuzungumza juu ya mkataba wake.

“Unajua maisha ya mchezaji ni mpira sasa kama Yanga watakuwa siriazi kuipata saini ya Aiyee tupo tayari kuwapa bure ila wawe na masalahi bora kwa mchezaji.

“Kwa sasa tunaendeea kupambana ambapo tunakwenda kumenayan a Geita mchezo wetu wa play off tutapambana kupata matokeo na kubaki kwenye ligi msimu ujao,” amesema.

UKIACHANA NA WALE WANAOTEMWA YANGA, HAWA HAPA WANATOLEWA KWA MKOPO KIBA ATAJA SABABU YA NIFUATE PROJECT, JUNI 2 KUWAKA TAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply