Uncategorized

MZEE AKILIMALI ATOA TAMKO JUU YA ROSTAM AZIZ, AUNGANA NAYE

admin June 23, 2019 8:10 am


Mjumbe wa Baraza la Wazee Yanga, Mzee Ibrahim Akilimali ‘Mzee Akilimali’ ambaye ni Katibu ameunga mkono hoja ya Rostam na kusema Yanga haiwezi kumilikiwa na mtu mmoja.

“Kwa kweli mimi nimefurahishwa na kauli ya Rostam na ninamkubali sana kwani klabu kubwa kama Yanga ambayo ina wanachama wengi huwezi kuimilikisha na mtu mmoja kwani kufanya hivyo ina maana kila kitu atakuwa nacho yeye.

“Mimi jana nilimsikiliza mwenyewe na timu kama Yanga inatakiwa iongozwe na wanachama sasa kama mwanachama umeenda pale na kudhani kuwa kuna mdhamini uache kuchangia basi wewe hufahi kuwa mwanachama, mwanachama unatakiwa uchangie.”

Kauli ya Akilimali imekuja mara baada ya Rostam kuibuka na kusema anataka kuifadhili Yanga kupitia makampuni yake na si kuimiliki.

AFANDE SELE AZICHANA VIBAYA SIMBA NA YANGA ‘HAWANA KWAO’ – VIDEO ROSTAM AWA MFALME YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply