BRUCE Kangwa, beki wa timu ya Azam FC amesema kuwa kilichowaponza kushindwa kutetea kombe la Kagame ni kushindwa kutumia nafasi walizozipata kwa umakini.
Azam FC ilifungwa bao 1-0 na KCCA kwenye mchezo wa fainali iliyochezwa nchini Rwanda na kuvuliwa ubingwa waliokuwa wanautetea.
Bruce Kangwa amesema:” Tulicheza kwa juhudi ndio maana tumefika hatua ya fainali, kikubwa kilichotuponza ni kutokuwa makini hicho tu ndicho kimetukosesha ubingwa,”.






