Home Uncategorized TANZANIA YAANZA KWA KUCHECHEMEA MICHUANO YA CECAFA

TANZANIA YAANZA KWA KUCHECHEMEA MICHUANO YA CECAFA

151
0

KIKOSI cha Timu ya Taifa ya Tanzania Chini ya Miaka 15 leo kimeanza kwa kuchechemea mbele ya Uganda kwa kupoteza mchezo wa kwanza kwa kufungwa mabao 2-0.

Tanzania ambayo inashiriki michuano ya CECAFA kwa timu za Vijana chini ya Miaka 15 imepangwa kundi B na leo imetupa kete yake ya kwanza.

Michuano hiyo inafanyika nchini Eritrea uwanja wa Asmara imeanza Agosti 16 na itakamilika Agosti 30.