Uncategorized

IBRAHIM AJIBU ATOA LA MOYONI KWA YANGA

admin July 5, 2019 6:31 am

BAADA ya kujiunga na Simba kwa kandarasi ya miaka miwili akitokea Yanga, aliyekuwa nahodha wa Yanga amewashukuru mashabiki na viongozi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika ujumbe huu:-

“Hakika ilikuwa miaka miwili bora sana kwangu, ndani na nje ya uwanja, Yanga ilikua sehemu ya familia yangu.

“Nitoe shukrani zangu za dhati kwa viongozi, benchi la ufundi, wachezaji na mashabiki kwa kuniamini na kuniunga mkono katika kila jambo.

“Ni mengi nimejifunza na nina amini yatanisaidia kunijenga zaidi kama wachezaji, asante sana, hadi wakati mwingine tena, wananchi, asante,” amesema Ajibu. 

NYOTA WA BONGO ATIMKIA KENYA ROSE MUHANDO MAJANGA TENA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply