Home Uncategorized ASHLEY YOUNG APEWA KITAMBAA CHA UNAHODHA UNITED

ASHLEY YOUNG APEWA KITAMBAA CHA UNAHODHA UNITED


OLE Gunnar Solskjaer, Meneja wa Manchester United amechagua jina la Ashley Young mwenye umri wa miaka 34 kuwa nahodha wa kikosi hicho.

Beki huyo alikuwa mpambanaji msimu uliopita ndani ya Old Trafford na amewaacha Paul Pogba, Nemanja Matic pamoja na Chris Smalling ambao walikuwa na nafasi za kuvaa kitambaa hicho.

Young kwa sasa ameongeza kandarasi ya mwaka mmoja ndani ya United ambacho alijiunga nacho mwaka 2011 akitokea Aston Villa kwa dau la pauni milioni 17.

Msimu uliopita alicheza jumla ya mechi 41 na kuchaguliwa kwake kumewashangaza wengi kwani kuna nyota kama Aaron Wan -Bissaka na Luke Shaw wote ni mabeki anakazi ya kuwa bora ili aanze kikosi cha kwanza msimu ujao.

SOMA NA HII  SAFU YA USHAMBULIAJI YA SIMBA YAISHTUA YANGA, MBINU YA KUIPOTEZA HII HAPA