Hamis Luwongo anayetuhumiwa kumuua na kumchoma moto mkewe, Naomi Marijani amezua kioja kingine Mahakamani Kisutu baada ya kuiomba mahakama impatie simu zake mbili, atoe pesa za kumsomesha mwanaye.
Mahakama imegoma kwa sababu simu hizo zinachunguzwa ikiwa kama sehemu ya upelelezi wa kesi yake inayomkabili.
Luwongo amerudishwa rumande na pingu miguuni kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi wa keshi hiyo.
Hivi karibuni aliwatishiwa waandishi wa habari mahakamani hapo akidai wanampiga picha kila wakati hivyo ipo siku atakuja kuwafanyia kitu mbaya cha kuishangaza mahakama lakini Hakimu alimweleza wanahabari wapo kwenye majukumu yao na ni haki yao kumpiga picha.
Credits. Global Publishers.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.