Home Uncategorized SIMBA YAWAITA MASHABIKI WAKE UWANJA WA TAIFA LEO

SIMBA YAWAITA MASHABIKI WAKE UWANJA WA TAIFA LEO


MSHAMBULIAJI wa Simba, Meddie Kagere amewataka mashabiki wa kikosi hicho wajitokeze kwa wingi leo uwanja wa Taifa kuipa sapoti timu hiyo itakapocheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Power Dynamo.

Simba leo inahitimisha kilele cha SportPesa Simba Wiki ambapo watacheza mchezo wa kirafiki uwanja wa Taifa na watatambulisha pia jezi na wachezaji wa Simba kwa ajili ya msimu mpya unaotarajiwa kuanza Agosti 23.

“Mashabiki wajitokeze kwa wingi kuona namna tutakavyofanya kweli mbele ya Power Dynamo kwani tumejipanga na tupo vizuri, mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti na tutatoa burudani ya kutosha,” amesema.

SOMA NA HII  POCHETTINO KUIBUKIA MANCHESTER UNITED IWAPO SOLSKJAER ATASHINDWA KUIFIKISHA HAPA