Uncategorized

MATOKEO MABAYA YAISIKITISHA YANGA, UJUMBE HUU WATUMWA SINGIDA

admin January 21, 2020 8:38 am


UONGOZI wa Yanga umesema kuwa umesikitishwa na matokeo ya mechi zake mbili zilizopita na kuomba sapoti kwa mashabiki wao.

Yanga iliyo chini ya Kocha Mkuu, Luc Eymael lipoteza mechi mbili mfululizo kwa kuchapwa mabao 3-0 na Kagera Sugar kisha ikapoteza kwa kufungwa bao 1-0 na Azam FC.

Ofisa uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema kuwa hawajafurahishwa a aina ya matokeo hayo mpaka sasa wanajipanga kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Singida United utakaochwezwa kesho, Namfua.

“Kwa matokeo ambayo tumeyapata tumesikitishwa na matokeo yaliyopita. Mashabiki wa Yanga wanapaswa kutokata tamaa, waendelee kuipa sapoti timu, sasa tunajipanga kumalizana na Singida United kwao,”  amesema Nugaz.

Yanga ipo nafasi ya nane kwenye msimamo ikiwa imejikusanyia jumla ya pointi 25 kibindoni.

SINGIDA UNITED BANA, YAITANGAZIA HATARI YANGA SVEN APINDUA UFALME WA MANULA, SASA KAKOLANYA ANAPETA KINOMA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply