Uncategorized

SINGIDA UNITED BANA, YAITANGAZIA HATARI YANGA

admin January 21, 2020 5:38 am


UONGOZI wa Singida United iliyo chini ya Kocha Mkuu, Ramadhan Nswanzurimo umesema kuwa hauna mashaka na mchezo wao wa kesho, Januari 22 dhidi ya Yanga utakaochezwa Uwanja wa Namfua, Singida.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Singida United, Cales Katemana amesema kuwa wanatambua mchezo utakuwa mgumu ila wamejipanga kupata ushindi.

“Tunatambua Yanga ni timu bora na ina wachezaji wenye uzoefu ila hilo halitupi mashaka tupo tayari kuona namna gani tutashinda.

“Mashabiki wajitokeze kutupa sapoti kwani timu imekuwa ikipita kwenye wakati mgumu ila kwa sasa tumeanza kurejea kwenye ubora,” amesema.

Singida United ipo nafasi ya 16 ina pointi 10 imeshinda mechi mbili pekee katika mechi 16 ilizocheza mpaka sasa.

JESHI LA AZAM FC LAKWEA PIPA KUIFUATA MWADUI FC MATOKEO MABAYA YAISIKITISHA YANGA, UJUMBE HUU WATUMWA SINGIDA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply