Uncategorized

SIRI YA AZAM FC KUIPIGA MWADUI HII HAPA

admin January 23, 2020 1:26 pm

UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa kikubwa kilichowapa ushindi jana mbele ya Mwadui FC ni kujituma kwa wachezaji.

Azam FC jana ilishinda bao 1-0 mbele ya Mwadui FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Kambarage.

Bao pekee la ushindi lilifungwa na Shaban Chilunda dakika ya 20 ya kipindi cha kwanza akimalizia pasi ya Nicolaus Wadada.

Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffary Maganga amesema kuwa ushindi walioupata umetokana na wachezaji kujituma ndani ya uwanja pamoja na morali waliyokuwa nayo.

“Wachezaji wana morali kubwa na walipambana kutafuta matokeo ndani ya uwanja mwisho wa siku wakapata kile walichokuwa wanakihitaji,” amesema.

MBELGIJI WA SIMBA ATEGUA MTEGO WAKE KIMTINDO RASMI, SAMATTA AANZA MAZOEZI ASTON VILLA AKIANDIKA REKODI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply