Uncategorized

SARE MBELE YA NDANDA YAWAFUNGUA MACHO AZAM FC, LEO KUWAVAA NAMUNGO KWA HESABU HIZI

admin February 22, 2020 3:41 am


IDD Cheche, Kocha Msaidizi wa Azam FC amesema kuwa makosa waliyoyafanya kwenye mchezo wao uliopita dhidi ya Ndanda FC wameyafanyia kazi hivyo watawavaa wapinzani wao namungo leo kwa mtindo wa kipekee.

Akizungumza na Saleh Jembe, Cheche amesema kuwa matokeo ya sare yaliwaumiza kwani walijipanga kupata pointi tatu kwa kuwa sare nayo ni sehemu ya mchezo imewapa somo ambalo limewawapa mbinu mpya.

“Tulikuwa tunahitaji pointi tatu mbele ya Ndanda kwa kuwa tumepoteza na kuambulia moja hakuna tatizo tunaendelea kupambana, makosa tuliyofanya mchezo uliopita tumeyafanyia kazi.

“Mashabiki tunawaomba wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti na kutazama ni namna gani tutatoa burudani na kupata ushindi mbele ya Namungo,” amesema.

Kabla ya kumenyana na Ndanda na kulazimisha sare, Azam FC ilikubali kichapo cha mabao 2-1 mbele ya Coastal Union, ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 45.

MBELGIJI APIGA CHINI MAPROO NDANI YA CHAMPIONI JUMAMOSI VUGUVUVUGU LA MACHI 8 LAWAZIBA MDOMO SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply