Home Uncategorized SIMCHIMBA AIOKOA AZAM FC USIKU MIKONONI MWA JKT TANZANIA

SIMCHIMBA AIOKOA AZAM FC USIKU MIKONONI MWA JKT TANZANIA


ANDREW Simchimba, mshambuliaji wa Azam FC jana ameiokoa timu yake usiku kuweza kusepa na pointi tatu mbele ya JKT Tanzania kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Bao hilo la ushindi lilifungwa dakika ya 90 na kuifanya JKT ipoteze matumaini ya kusepa na pointi moja kwenye mchezo huo ambao wao walikuwa wenyeji.

Azam FC inafikisha pointi 48 ikiwa imecheza mechi 25 inajikita nafasi ya pili huku kinara akiwa ni Simba mwenye pointi 62.

SOMA NA HII  YANGA IPO KAMILI GADO KUIVAA TANZANIA PRISONS