Home Uncategorized SINGIDA UNITED: TULIPASWA TUIFUNGE MABAO 5-0 POLISI TANZANIA, MAMBO BADO MAGUMU

SINGIDA UNITED: TULIPASWA TUIFUNGE MABAO 5-0 POLISI TANZANIA, MAMBO BADO MAGUMU


RAMADHAN Nswanzurimo, Kocha Mkuu wa Singida United amesema kuwa jana Februari 29 walipaswa waifunge Polisi Tanzania mabao 5-0 ila bahati haikuwa yao kutokana na wachezaji kushindwa kumalizia nafasi walizozipata.

Singida United ilipoteza mchezo wake kwa kufungwa bao 1-0 lililolofungwa na Sixtus Sabilo kwa mkwaju wa penalti huku mkwaju wa Singida United uliopigwa kutokana na mabeki kucheza faulo ndani ya 18 kupanguliwa na Manyika Jr.

Nswanzurimo amesem: “Siwezi kuingia ndani kucheza kwani tulipanga kumaliza mchezo mapema ndani ya kipindi cha kwanza mwisho wa siku ikawa ngumu.

“Tulipata nafasi za kufunga mabao matano na haijawa hivyo sina chaguo kwa kuwa matokeo yameshatokeo,”.

Singida United inaendelea kuburuza mkia ikiwa imecheza mechi 25 ina pointi 12 kibindoni.

SOMA NA HII  VIDEO:ILE ISHU YA NDEVU ZA KARANTINI ZA MORRISON HUKU NDIKO LILIKOTOKEA