Uncategorized

MBELGIJI WA YANGA AUKUBALI MUZIKI WA SIMBA

admin March 18, 2020 12:12 pm

KOCHA Mkuu wa Yanga, Luc Eymael amesema kuwa timu ya Simba ni miongoni mwa timu kubwa Bongo kutokana na uwezo wake wa kutokata tamaa ya kupambana.

Eymael alikiongoza kikosi chake cha Yanga kuinyoosha Simba kwa bao 1-0 walipokutana kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Machi 8 Uwanja wa Taifa.

“Simba ni timu kubwa imeweza kuleta ushindani kwenye ligi kwani iliweza kurejea kwenye mstari licha ya kuichapa bao 1-0 tulipokutana kwenye mchezo wetu wa ligi.

“Walifanikiwa kushinda mchezo wao uliofuata mbele ya Singida United kwa ushindi wa mabao mengi (8-0) hii inamaanisha kwamba waliweza kugundua makosa yao na kurejea kwenye ubora,” amesema Eymael.

Yanga baada ya kuitungua Simba kwa bao lililofungwa na Morrison Bernard imecheza mechi mbili na kuambulia pointi moja baada ya kupoteza mechi moja mbele ya KMC na sare ya kufungana bao 1-1 na Namungo.

ALIYEMBANA MEDDIE KAGERE ALIPEWA MBINU NA SIMBA WENYEWE WAWILI SASA NDANI YA JUVENTUS WATHIBITISHWA KUWA NA CORONA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply