Home Uncategorized HESABU ZA MBARAKA YUSUPH ZIPO NAMNA HII

HESABU ZA MBARAKA YUSUPH ZIPO NAMNA HII

MBARAKA Yusup

h, mshambuliaji wa Azam FC  amesema kuwa kwa sasa anaendelea na mazoezi binafsi akiwa nyumbani ili kurejea kwenye kasi yake ya zamani.


Mbaraka alikuwa nje kwa muda mrefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha, amerejea kikosini hakupata nafasi ya kucheza mpaka Ligi Kuu Bara iliposimamishwa kutokana na kuzuia maambukizi ya Virusi ya Corona.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mbaraka amesema kuwa amekuwa akiendelea na mazoezi nyumbani jambo ambalo anaamini litampa nafasi ya kurejea kwenye ubora.

“Ninaendelea na mazoezi binafsi nyumbani nina imani itakuwa na manufaa ya kurudisha kipaji changu kikubwa ni kuomba Mungu hali itulie kwa sasa.

“Changamoto kubwa ambayo tunapitia kwa sasa ni kushindwa kuwa uwanjani kwa pamoja lakini hamna namna ni lazima tujilinde na tufuate kanuni za afya,” amesema.

Azam FC ipo nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 54 baada ya kucheza mechi 28.
SOMA NA HII  KOCHA YANGA ATUA DAR KUMALIZANA NA MABOSI WAKE