Uncategorized

KISA YANGA, SIMBA YAMKOMALIA CHAMA, YATAJA MUDA WA MKATABA WAKE

admin April 14, 2020 2:27 pm


UONGOZI wa Simba umesema kuwa kiungo wao Clatous Chama raia wa Zambia mkataba wake bado unaishi mpaka pale Juni 2021.

Chama amekuwa akihusishwa kujiunga na wapinzani wa Simba Yanga ambao inaelezwa kuwa wameanza kufanya mazungumzo na nyota huyo ambaye kwa sasa yupo nchiniZambia.

Ofisa Habari wa Simba Haji Manara amekanusha taarifa kuhusu mkataba wa kiungo  Chama kumalizika mwaka huu, akisisitiza kuwa mkataba wa nyota huyo utamalizika mwezi Juni mwaka 2021.

“Timu yoyote itakayoanza kufanya mazungumzo na Chama itakuwa ni kinyume na utaratibu wa Shirikisho la Soka duniani (Fifa) hivyo walioanza waache mara moja.

“Tunajua kwamba ni mchezaji mzuri lakini bado ni mali ya Simba kwa sasa labda kama walikuwa hawajui bado ni mali yetu na haendi popote pale,” amesema.

BANDA:TUNAPIGA MATIZI KAMA KAWAIDA HUKU CHELSEA YAWEKA NGUMU KWA KANTE KUIBUKIA KWA ZIDANE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply