Uncategorized

NYOTA HUYU KIPENZI CHA MASHABIKI ATAJWA KUREJEA JANGWANI

admin April 18, 2020 6:31 am

INAELEZWA kuwa miongoni mwa washambuliaji ambao wanahitajika kurudi ndani ya Klabu ya Yanga ni pamoja na staa wao wa zamani, Heritier Makambo anayekipiga Horoya.

Msimu wa 2018/19 Makambo alifanya kazi kubwa ndani ya Yanga akiwa ametupia mabao 17 huku kinara akiwa na Meddie Kagere aliyetupia mabao 23.

Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa kuhusu suala la Makambo muda utazungumza kwani ni mchezaji anayependwa na Yanga.

“Makambo ni mchezaji mzuri na anapendwa hivyo hilo ni suala la kusubiri na kuona mambo yatakuaje, ila kwa sasa tuache bado muda wake haujafika,” amesema.

CHAMA ATAJA HATMA YAKE NDANI YA SIMBA MORRISON BALAA LAKE LILIKUWA NAMNA HII NDANI YA LIGI KUU BARA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply