Uncategorized

KUMEKUCHA JANGWANI, YAMALIZANA NA JEMBE HILI LA KINYARWANDA

admin May 26, 2020 1:47 pm

WAKIWA tayari wana majina ya Michael Sarpong na Jules Ulimwengu wanaocheza Rwanda, wadhamini wa Yanga, Kampuni ya GSM, wamefanya jambo kubwa lingine kwa kuipa mkataba mashine mpya ya Kinyarwanda ambayo itatua klabuni hapo msimu ujao.
Mabosi hao wa GSM wamemalizana na kumpa mkataba beki wa kushoto Erick Rutanga ambaye kwa misimu miwili Yanga walikuwa wakimfuatilia lakini walishindwa kumnasa baada ya Rayon Sports kumpa mkataba.
Beki huyo anakuja kuongeza nguvu kwenye upande wa kushoto wa Yanga ambao kwa msimu huu unawategemea zaidi Japhary Mohammed na Adeyum Saleh.

Habari zilizothibitishwa na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GSM, Injinia Hersi Said ni kuwa beki huyo tayari kila kitu kimeenda sawa na kinachosubiriwa ni ligi kumalizika kisha beki huyo atue Jangwani.
“Kila kitu kuhusiana na beki huyo wa kushoto kimeenda sawa na kinachosubiriwa ni kuja kujiunga na timu kwa msimu ujao baada ya kukubaliana kwenye mambo ya msingi aliyoyataka.
“Kwa muda mrefu alikuwa kwenye tageti zetu lakini alisaini mkataba na Rayon misimu miwili nyuma na sasa anaenda kumaliza mkataba wake kwa hiyo tulichofanya ni kumuwahi kabisa kwa kukubaliana naye.
“Atakuja kuungana na wale wengine ambao tumetangaza tayari tumemalizana nao na wale ambao tuko kwenye mazungumzo ya mwisho kwa ajili ya msimu ujao kutua kikosini kwetu,” alisema Hersi.

Chanzo:Championi
MWENYEKITI BIASHARA UNITED: TULIKUWA NA HALI MBAYA SANA VIDEO:MWENYEKITI WA ZAMANI WA SIMBA ADEN RAGE ASIMULIA ALIVYOKAMATWA NA TAKUKURU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply