Home Uncategorized SABABU YA MEDDIE KAGERE KUWEKWA KWENYE RADA ZA TIMU YA HISPANIA HII...

SABABU YA MEDDIE KAGERE KUWEKWA KWENYE RADA ZA TIMU YA HISPANIA HII HAPA

MEDDIE Kagere, mshambuliaji namba moja ndani ya Klabu ya Simba alitajwa kuibukia ndani ya Klabu ya Levante ya Hispania.

Inaelezwa kuwa sababu kubwa ya nyota huyo kuingia kwenye rada za vigogo hao wa Hispania ni mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliochezwa Uwanja wa Taifa kati ya Simba na Sevilla.

Mechi hiyo ilikamilika kwa Simba kunyooshwa kwa mabao 5-4 huku Kagere akifunga bao moja na kutoa pasi kwa John Bocco ambaye ni nahodha wa Simba.

Kagere aliwekwa kwenye rada za mabosi hao ambao walikuwa wanahitaji saini yake ila kwa sasa hawajaibuka tena kukumbusha dili lao.

SOMA NA HII  MESSI ANATAKA KUSEPA BARCELONA