Uncategorized

HAPA NDIPO LILIPO TATIZO LA MBEYA CITY

admin June 22, 2020 2:47 pm


AMRI Said, Kocha Mkuu wa Mbeya City amesema kuwa mfumo wake wa kucheza mipira mirefu ni tatizo jambo ambalo analifanyia kazi kwenye mechi zake zinazofuata.

Juni 20, Mbeya City ilikubali kichapo cha bao 1-0 mbele ya Alliance kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Sokoine.

Ana kibarua kingine tena Juni 24 Uwanja wa Sokoine kumenyana na Simba ambayo tayari imeshatia timu ndani ya jiji la Mbeya.

 Said amesema:”Wachezaji wangu walikuwa na kazi kubwa kwenye mchezo wetu dhidi ya Alliance kuendana sawa na mfumo ule wa mipira mirefu jambo ambalo liliwapa shinda hasa kwa namna ya kuzuia mashambulizi ila kwa kuwa mchezo wetu umeshapita tunajipanga kwa ajili ya mechi zinazofuata.”

Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa, Mbeya City ilalala kwa kuchapwa mabao 4-0 wakati ule ikiwa chini ya Kocha Mkuu, Juma Mwambusi.

NAMUNGO SASA KUKIWASHA MOTO NA YANGA TAIFA POLISI TANZANIA BADO HAIJAREJEA KWENYE UBORA WAKE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6131

Leave a Reply