LILE shindano la wasomaji wa magazeti bora ya michezo zilizofanyiwa uchunguzi wa kina, Championi na Spoti Xtra, ambapo mshindi anatarajiwa kukabidhiwa gari jipya aina ya Toyota FunCargo sasa linaelekea ukingoni kwa ajili ya mshindi kukabidhiwa ndinga hiyo.
Jana Alhamisi, Kitengo cha Masoko na Usambazaji cha magazeti hayo, kilitua mitaani maeneo mbalimbali ya Tegeta jijini Dar kwa ajili ya kuendelea kuwahamasisha wasomaji hao kuzidi kununua magazeti hayo na kukata kuponi iliyopo ukurasa wa pili wa magazeti hayo kwa ajili ya kushiriki bahati nasibu hiyo.
Akizungumza na wasomaji hao Mkuu wa Kitego hicho, Anthony Adam aliwaambia wasomaji hao wazidi kushiriki shindano hilo kwani gari hiyo inatarajiwa kukabidhiwa kwa mshindi mapema mwezi ujao.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.