Home Uncategorized WINGA SIMBA AIBUKIA POLISI TANZANIA

WINGA SIMBA AIBUKIA POLISI TANZANIA

0

 

RASHID Juma, winga wa Simba amejiunga na Klabu ya Polisi Tanzania kwa mkopo kwa wa mwaka mmoja.

Nyota huyo msimu wa 2020/21 atakuwa ndani ya Polisi Tanzania yenye maskani yake Kilimanjaro.

Ndani ya Simba ambao ni mabingwa watetezi hakupata nafasi ya kuwika kwa msimu wa 2019/20 kutokana na ufinyu wa namba.

Pia ilipaswa atolewe kwa mkopo msimu uliopita ila nyota huyo inaelezwa kuwa hakuwa tayari ila msimu huu amekubali kuibukia ndani ya Polisi Tanzania .