Home Uncategorized KIUNGO ‘ALIYEJIFUNGA’ MIAKA MINNE YANGA ANA TUZO MKONONI

KIUNGO ‘ALIYEJIFUNGA’ MIAKA MINNE YANGA ANA TUZO MKONONI

 Feisal Salum kiungo ndani ya Klabu ya Yanga kwa mujibu wa Injinia Hersi Said Mkurugenzi wa Uwekezaji kampuni ya GSM ambao ni wadhamini wa Klabu hiyo amesema kuwa ameongeza mkataba wa miaka minne.
Kwa maana hiyo Feisal atakuwa ni mali ya Yanga mpaka 2024 kwa timu itakayokuwa inasaka saini yake lazima ijipange kuweka mkwanja mezani.

Kwa msimu wa 2019/20, Feisal amekuwa bora ndani ya Ligi Kuu Bara akianza kikosi cha Kwanza kwenye jumla ya mechi 22.

Ana tuzo ya mchezaji bora ndani ya Yanga aliyokabidhiwa na wadhamini wakuu wa Klabu hiyo, kampuni ya SportPesa.

Amefunga bao moja ndani ya ligi msimu huu ilikuwa Uwanja wa Mkapa dhidi ya Mwadui FC kwenye sare ya kufungana bao 1-1.

SOMA NA HII  PILATO WA DABI YA YANGA V SIMBA HUYU HAPA