Home Uncategorized MZUNGUKO WA KWANZA VPL NOMA,MABAO 14 YAFUNGWA,KMC BABA LAO

MZUNGUKO WA KWANZA VPL NOMA,MABAO 14 YAFUNGWA,KMC BABA LAO

0

MZUNGUKOwa Kwanza kwa msimu wa 2020/21 umekamilika jana Septemba 7 baada ya kuanza kwa Ligi Kuu Bara Septemba 6.

Jumla ya mabao 14 yamefungwa katika mechi 9 za mzunguko wa kwanza huku KMC wakiwa wa kwanza kutoa dozi nene ya mabao 4-0 mbele ya Mbeya Mbeya City.

Timu saba zimeshinda, timu saba zimepigwa, timu nne zimetoka sare. Walioshinda ugenini ni Simba na JKT Tanzania pekee huku timu nane zikiwa hazijaruhusu goli lolote.