Home Uncategorized JEMBE JIPYA SIMBA HATMA YAKE MIKONONI MWA SVEN

JEMBE JIPYA SIMBA HATMA YAKE MIKONONI MWA SVEN


 IBRAHIM Ame, beki mpya ndani ya kikosi cha Simba hatma yake ya kuwavaa Ihefu leo ipo mikononi mwa Kocha Mkuu Sven Vandenbroeck kwa kuwa alikuwa anasumbuliwa na majeraha.

Leo Septemba 6, Simba ambao ni mabingwa watetezi watarusha kete yao ya kwanza, Uwanja wa Sokoine dhidi ya Ihefu kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara alisema kuwa maendeleo ya Ame yapo vizuri kwa kuwa tayari alishaanza mazoezi na wachezaji wenzanke.

“Ame kwa sasa anaendelea vizuri na tayari alishaanza kufanya mazoezi na wachezaji wenzake. Alikuwa na majeraha aliyoyapata kwenye mchezo dhidi ya AFC Arusha ila kwa sasa yupo vizuri maamuzi ya kocha tu yanasubiriwa kuanza kwenye mechi za ushindani,” alisema.

 

SOMA NA HII  KIUNGO FUNDI WA SIMBA SASA KUIBUKIA YANGA, APIGWA MIAKA MIWILI