Simba inaondoka leo Lagos kuifuata Plateau katika mji wenye makao makuu yake. Umbali zaidi ya Kilomita 300 na Simba imeshauriwa kutumia ndege kwa kuwa katikati ya miji hiyo kumekuwa na matukio ya utekaji watu.
Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Dk Benson Bana amekuwa kati ya watu waliotilia mkazo suala hilo la kutumia usafiri wa ndege.